Kujitambua ni ile hali ya mtu kujijua au kujielewa yeye ni
nani, ana thamani gani, na umuhimu wake katika jamii anayoishi. Ni kuwa na
uwezo wa kujua au kuelewa vipaji mbalimbali ambavyo Mungu amekujalia na uwezo
wako wa kufanya mambo mbalimbali.Baadhi ya vipaji ni kama kuimba ,kufundisha
,uongozi,ufundi,biashara n.k
Pia kuelewa udhaifu ulionao kama binadamu na hivyo
kujiepusha kuwa chanzo au chachu ya migogoro katika jamii unayoishi.Baadhi ya
madhaifu ni :Hasira ,umbea,gubu,kisirani,ufitini,n.k
Ni kuwa na uwezo wa kuelewa nafasi yako na umuhimu wako
katika jamii unayo ishi.Ni muhimu kutambua jamii inakuelewaje,una hekima au
hapana;Ni kuwa na uwezo wa kuchambua malengo yako ya maisha na
kuona kwamba ni halisi yanawezekana au hapana pamoja na kujiwekea mikakati ya
kufanya ufanikiwe.
Ni kuwa na uwezo wa kutambua mambo yanayo kuogopesha katika
maisha yako na sababu zake mfano:unaogopa kifo na kwanini unaogopa;Kuwa na upeo wa kuchambua aina ya watu unaopenda kuwa
nao,wakiwa marafiki.Na kujaribu kujiuliza kila wakati,Je?marafiki ulionao ni wa
sifa hizo?
Kwa
kifupi naweza kusema kujitambua ni hali ya kuwa na ufahamu wa nini kuhusu
wewe.Hali yako,umuhimu wako,malengo yako,hatima yako, changamoto zako, nk, hayo
yote yanakuwa wazi kwako kwa kujitambua.
![]() |
| Reality vs Imagination. |

No comments:
Post a Comment