1. Programu ya Wezeshwa iko wazi kwa Mtanzania yeyote mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 40 na awe anaishi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
2.Nakala ya Kitambulisho cha mshiriki lazima kiambatanishwe na fomu ya usajili.
3.Ushiriki ni wa hiari na utanzingatia kanuni na maelekezo ya Programu.
4. Ukusanyaji wa fomu za programu utamalizika tarehe 15 February 2013, na fomu zote za ushiriki lazima zirudishwe katika vituo vilivyopangwa kabla ya saa 11 jioni ya siku hiyo.
5. Kampuni ya Tanzania Breweries Ltd haitawajibika kwa upotevu wa fomu za ushiriki au nakala za nyaraka zinazohusu programu hii.
6. Fomu ambazo hazijakidhi vigezo vilivyowekwa hazitazingatiwa.
7. Ni lazima mshiriki awe anaendesha na kusimamia biashara yake kwa muda wote.
8.Vigezo na masharti kuzingatiwa,Uamuzi wa majaji wa Programu hii ni uamuzi wa mwisho.
9. Kwa kukubali kushiriki na Programu hii ya TBL ina haki ya kutoa matangazo magazetini, kuchapisha majina na picha za
washiriki na washindi wa shindano na pia kufanya nao mahojiano bila malipo ya ziada.
10.Waratibu wa Programu ya Wezeshwa wataendelea kukagua maendeleo ya biashara zinazoendeshwa na washindi pale
itakapo lazimu kwa angalau kipindi cha miaka mitano (5).
11. Kanuni za ushiriki hazitabadilishwa wakati wa Programu.
